Transfer News

Maduka ya kamari yameweka dau la kuashiria kuna uwezekano mkubwa wa Harry ane kuondoka Tottenham na kwenda Manchester United (Daily Star). Hata hivyo Tottenham wametupilia mbali uwezekano wa Harry Kane kwenda Old Trafford na kusema thamani ya mshambuliaji wao ni karibu pauni milioni 200 (Independent). Alex Sandro, 26, amekubali kujiunga na Chelsea huku mabingwa hao wa England wakikaribia kukamilisha mkataba wa pauni milioni 61 kumsajili beki huyo wa Juventus (Corriere della Sera). Sandro huenda akaungana na Virgil van Dijk, 25, kutoka Southampton, na mshambuliaji Romelu Lukaku, 24, kutoka Everton na kiungo mkabaji wa Monaco Tiemoue Bakayoko, 22, wakati Chelsea ikijiandaa kutumia pauni milioni 240 msimu huu (Daily Express). Arsenal na Manchester City wanafikiria kubadilishana washambuliaji, Alexis Sanchez, 28, kwa Sergio Aguero, 29 (Daily Star). Hata hivyo Alexis Sanchez ameshawishiwa na mchezaji mwenzake wa timu ya taifa, Arturo Vidal, kwa kuambiwa aachane na Arsenal na kwenda ...